Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Idara ya Mahusiano ya Umma ya Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) imetangaza kuwa katika kipindi cha saa 24 zilizopita, jumla ya meli 28, zikiwemo meli za kubeba mafuta na makontena, zimevuka Mlango wa Bahari wa Hormuz baada ya kuratibiwa mapema na kupata vibali vinavyohitajika kutoka kwa mamlaka husika.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, shughuli za usimamizi na ufuatiliaji katika Mlango wa Hormuz zinaendelea kufanyika kwa kutumia mifumo ya kisasa ya uangalizi wa kielektroniki, kwa lengo la kuhakikisha usalama wa njia hiyo muhimu ya kimataifa ya usafirishaji wa bidhaa na nishati.
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu limesisitiza kuwa ufuatiliaji wa Mlango wa Hormuz unaendelea kwa umakini, uthabiti na ufanisi mkubwa, ili kudumisha usalama wa meli zinazopita katika eneo hilo na kulinda maslahi ya usafiri wa baharini.
Your Comment